Social Icons

Monday, February 21, 2011

MAKAMU WA RAIS APOKEA UJUMBE KUTOKA KWA RAIS MUGABE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohamed Gharib Bilal, akisalimiana na Naibu Waziri Mkuu wa Zimbabwe Mhe. Thokozani Khupe wakati Naibu waziri huyo alipofika Ofisini kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es salaam leo, kwa ajili ya kumkabidhi ujumbe maalum wa Rais Kikwete kutoka kwa Rais wa Zimbabwe Mhe. Robert Mugabe unaoelezea juu ya maendeleo na maandalizi ya Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika miaka miwili ijayo Nchini Humo.

Dk. Mohamed Gharib Bilal, akizungumza na Naibu Waziri Mkuu wa Zimbabwe Mhe. Thokozani Khupe. Alipofika Ofisi kwa Makamu wa Rais Ikulu Dar es salaam leo, kwa ajili ya kumkabidhi Ujumbe Maalum wa Rais Kikwete, kutoka kwa Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe.

Picha kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais.

0 comments: