Social Icons

Friday, December 31, 2010

GLOBAL PUBLISHERS WAOMBA DUA YA KUFUNGA MWAKA


Baadhi ya wafanyakazi hao wakiwa kwenye maombi hayo.

WAFANYAKAZI wa kampuni ya Global Publishers, wachapishaji wa magazeti ya Ijumaa, Risasi, Championi, Amani, Ijumaa Wikienda na Uwazi, asubuhi ya leo wamekusanyika pamoja makao makuu ya ofisi hizo eneo la Bamaga, Sinza, jijini Dar es Salaam, na kuendesha sala na dua ya kufunga mwaka wa 2010. Hili lilifanyika muda mfupi baada ya kumaliza kikao cha kupitia magazeti yaliyotoka leo.
Mtaalam wa IT wa kampuni hiyo Clarence Mulisa (kushoto), akishiriki sala hiyo na Mhariri wa gazeti la Amani, Hamida Hassan. Kushoto zaidi ni mkuu wa wachoraji katuni wa kampuni hiyo, Aloys James.
Mhariri wa gazeti la Championi Ijumaa, Elius Kambili (kushoto), akiwa kwenye pozi na Mhariri wa gazeti la Championi Jumatatu, Philip Nkini (katikati) muda mfupi baada ya maombi hayo kumalizika, na kulia ni mwandishi wa magazeti pendwa, Shakoor Jongo.
Mhariri kiongozi wa magazeti ya Championi, Saleh Ally (kushoto), akiwa kwenye pozi na wahariri wa magazeti hayo.

0 comments: