Social Icons

Monday, August 29, 2011

JAPAN YAIPA TANZANIA BILIONI 40 KWA AJILI YA UJENZI WA DARAJA LA LUSUMO NA BARABARA JIJINI DAR

Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (leo) jijini Dar es salaam mara baada ya kusaini msaada wa shilingi bilioni 40 kwa ajili ya miradi miwili ya maendeleo. Mradi wa kwanza ni ujenzi wa daraja la Rusumo lilopo mpakani wa Tanzania na Rwanda na uimarishaji wa barabara jijini Dar es salaam. kulia ni Balozi wa Japan nchini Hiroshi Nakagawa.

Picha/Habari na Tiganya Vincent,

Hadija Chumu na Moshi Stewart-Maelezo

Dar es Salaam

SERIKALI imesaini msaada wa shilingi bilioni 40 na serikali ya Japan kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa miradi miwili ya maendeleo hapa nchini.

Akiongea na wanahabari leo Waziri wa Fedha na Uchumi Mustapha Mkulo amesema, miradi hiyo ni ya ujenzi la wa daraja la Rusumo litakalounganisha nchi ya Tanzania na Rwanda na upanuzi wa barabara ya Kilwa ambapo itasaidia shughuli za maendeleo baina ya nchi hizo.

Waziri Mkulo alisema

Alisema upanuzi wa barabara ya kilwa utapunguza kwa kiasi kikubwa foleni na adha nyingine za kimiundombinu ndaji ya jiji la Dar es salaam,

Nae Balozi wa Japani nchini Bw Hiroshi Nakagawa amesema msaada huo ni matokeo ya ushirikiano uliopo kati ya Japani na Tanzania ambapo utasaidia kuimarisha uchukuzi na usafirishaji nchini,

Balozi Nakagawa alisema kiasi cha bilioni 1.86 za kijapani zitasaidia upanuzi wa daraja la Rusumo, wakati Yen Milioni 37 zimetolewa kukamilisha upanuzi wa barabara ya kilwa

Nae mwakilishi wa shirika la JICA nchini Bw Yukihide Katsuta amesema fedha zilizotolewa na shirika hilo ni milioni 769 za kitanzania ambazo zitasaidia kupata mwongozo sahihi wa kitaalam utakaopelekea ubora katika ujenzi na upanuzi wa barabara ya kilwa unaotegemea kukamilika hivi karibuni

Aidha mwakilishi wa TANROADS Mhandisi Mfugale amesema watahakikisha mradi huo unatekelezwa kwa wakati na ubora unaohitajika ili kuhakikisha na kusimamia upanuzi wa daraja hilo pamoja na ule wa upanuzi wa barabara ya kilwa unatimizwa kulingana na fedha zinazotolewa.

0 comments: