Social Icons

Monday, March 28, 2011

MIRIAM LUKINDO ATAMBULISHA VIDEO YA ALBAMU YAKE

Tunu Pinda akiingia ndani ya ukumbi wa Blue Pearl huku akisalimiana na mke wa Waziri Mkuu wa zamani, Bi Regina Lowassa.

MWIMBAJI wa nyimbo za Injili nchini, Miriam Lukindo, jana alitambulisha video ya albamu yake ijulikanayo kama “Ni Asubuhi” kwa baadhi ya viongozi wa serikali na wabunge katika ukumbi wa Blue Pearl, jijini Dar es Salaam. Uzinduzi kamili wa video hiyo utafanyika tarehe 10 Aprili mwaka huu kwenye ukumbi wa Diamond, pia jijini Dar es Salaam.Miongoni mwa viongozi waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda, aliyekuwa mgeni rasmi.



Mama Tunu Pinda (wa kwanza kushoto) akiwa na Miriam Lukindo (katikati), kulia ni Bi Regina Lowassa.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Vicky Kamata (kushoto), akifuatilia hafla hiyo.

Miriam Lukindo akiwajibika kwenye jukwaa.

Wageni katika hafla hiyo wakiserebuka na wimbo wa Miriam Lukindo unaoitwa ‘Amen’.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Martha Mlacha (kulia), akicheza kwa hamasa.

Tunu Pinda akiitambulisha rasmi albamu ya “Ni Asubuhi”.

Regina Lowassa akipakua msosi katika hafla hiyo.

0 comments: