Social Icons

Monday, March 28, 2011

MAPACHA 3 WANADI TUZO ZAO KWA MASHABIKI

Mwanamuziki wa bendi hiyo Jose Mara aki... kwa furaha na mke wake muda mfupi baada ya kuanza kunadi tuzo hizo.

Baba wa Kalala Junior wa pili kutoka kulia, Komando Hamza Kalala, akiongea jambo kuhusiana na tuzo za wanae.

Mwanamuziki wa bendi hiyo Kalala Junior (kulia), akiwa amenyanyua juu moja ya kadi aliyozawadiwa na mashabiki zake, kushoto kwake ni Jose Mara na Khald Chokora wakiwa na maua mkononi pamoja na tuzo hizo.

Baadhi ya wapenzi wa bendi hiyo wakiwapongeza Mapacha Watatu kwa kutwaa tuzo hizo.
Meneja wa Bendi hiyo, Khamis Dakota, akifurahia kutwaa tuzo hiyo.
Kimwana Manywere 2007, Husna Idd 'Sajenti' (kulia), akifuatilia mchakato mzima wa kunadi tuzo za Mapacha Watatu na rafiki yake.
Sajenti akifuatilia kwa makini Swagger za bendi hiyo.

BENDI ya Muziki wa dansi Bongo, inayoundwa na vichwa vitatu Khald Chuma 'Chokoraa', Joseph Michael 'Jose Mara, na Junior Hamza 'Kalala Junior', maarufu kwa jina la Mapacha Watatu, Usiku wa kuamkia leo, waliweza kunadi tuzo walizotunukiwa na Kili Music Awards, jumamosi iliyopita ndani ya Ukumbi wa Diamond Jublee.

Ishu hiyo ya kunadi tuzo zao ilifanyika katika Ukumbi wa Mzalendo Pub ndani ya Jengo la Millenium Tower, Kijitonyama jijini Dar es Salaam, ambapo bendi hiyo hufanya shoo zake kila siku ya jumapili.

Bendi hiyo ilijinyakulia tuzo ya Wimbo Bora wa Kiswahili na Rapa Bora kwa upande wa bendi ambayo alitwaa kiongozi wa bendi hiyo Khald Chuma 'Chokoraa'.

0 comments: