Social Icons

Thursday, February 24, 2011


Meneja masoko wa Airtel, Kelvin Twissa akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari.
Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi ya Airtel, leo imetangaza huduma yake mpya itakayofahamika kwa jina la Airtel Flava.

Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya kampuni hiyo yaliyopo Kinondoni Moroco jijini Dar es Salaam, meneja masoko wa Airtel Kelvin Twissa alisema kwamba, huduma hiyo itakuwa mahususi kwa kuchangamsha huduma za wateja wao.

Twissa alisema kuwa, kupitia huduma hiyo wateja wote wa Airtel wataweza kujichagulia muziki wowote na kuusikiliza kupitia simu zao wakati wowote kwa kupiga namba 15565 na kuchagua muziki husika.



Baadhi ya waandishi wa habari wakinakili baadhi ya maelezo kutoka kwa meneja huyo.


Meneja wa huduma za ziada wa Airtel, Frank Semaganga akifafanua namna ya kuitumia huduma hiyo.

0 comments: