Social Icons

Monday, February 21, 2011

KILI YAWEKA HAZALANI MAJINA YA WATAKAO WANIA TUZO

Meneja wa Kinywaji cha Kilimanjaro George Kavishe, akiongea jambo kwa Waandishi wa Habari.
Lloyd 2hungu, kutoka kampuni ya Innovey Auditors (kulia), akimkabidhi kalatasi yenye majina ya waliochaguliwa kuwania tuzo hizo, Mratibu wa Tuzo za Kilimanjaro Musica Awards, kutoka Baraza la Sanaa Tanzania ( BASATA), Angelo Luhala.
Angelo Luhala akisoma majina ya washirki wa tuzo hizo.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakijaribu kuweka kumbukumbu za tukio hilo.

KAMPUNI ya vinywaji ya Tanzania Bruwers Limited (TBL) kupitia kinywaji chake cha Kilimanjaro, ambayo ndiyo inadhamini tuzo za Kilimanjaro Musica Awards 2011.
Mapema leo imetangaza majina ya wasanii watakao wania tuzo hizo. Tukio la kutaja kwa majina hayo lilifanyika Makao makuu ya ofisi hizo Ilala jijini Dar es Salaam, chini ya meneja wa kinywaji hicho George Kavishe na mratibu wa tuzo hizo kutoka Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), Angelo Luhala. Akizungumza mbele ya waandishi wa Habari Kavishe alisema kuwa majina hayo yamependekezwa chini ya usimamizi wa kampuni ya Innovex Auditors, huku majina hayo yakikabidhiwa kwa mmoja wa wahusika kutoka kampuni hiyo Lloyd Thungu. Luhala alianza kwa kutaja wasanii watakao shindana kuwania tuzo ya msanii wa kike bora kwa mwaka huu watachuana kati ya Judith Wambura “Lady Jay Dee”, Mwasiti Almasi, Astelina Sanga ‘Linah’, Salah Kaisi ‘Shaa’ na Khadija Omari Kopa ‘Khadija Kopa’. Kwa upande wa msanii Bora wa kiume ni ‘20%’, Ali Kiba, Elius Barnaba, Naseeb Abdull ‘Diamond’, Ambwene Yeseya ‘AY’ na Bell 9. Mwimbaji Bora wa Kiume ni ‘20%’, Barnaba, Ali Kiba’ Banana Zorro, Bell 9 na Diamond. Mwimbaji Bora wa Kike ni Lady Jay Dee, Linah, Mwasiti, Khadija Kopa na Shaa. Wimbo Bora wa Taarab My Valentine wa Jahazi Modern, Top in Town wa Khadija Kopa, Achani Kuniandama Isha Ramadhani Mashauzi Langu Rohini Jahazi Morden na Mama nipe Radhi wa Isha Mashauzi. Wimbo Bora wa Mwaka Mama Ntilie Gelly wa ryames feat AT & Ray C, Sina Raha Sam wa Ukweli, Ya Nini Malumbano 20%, Mkono mmoja Chege & Temba Feat Wahu, Bado Tunapanda Tip Top Conection na Tamaa Mbaya 20%. Wimbo Bora wa Kiswahili (Bandi) Shika ushikapo Mapacha watatu feat Mzee Yusuf, Laptop Extra Bongo, Kauli Twanga Pepeta, Mapenzi hayana Kiapo Twanga Pepeta na Pongezi kwa wanadoa Akudo Impact. Wimbo Bora wa R&B We ni wangu Bell 9, Nikikupata Ben Poul, Hello Hussein Machozi feat Maunda Zorro , Atatamani Linah na Kisiwa cha Malavidavi Z Anton. Wimbo Bora wa Hip Hop Propaganda wa Fid Q, Karibu Tena wa John Makini,Ukisikia Paah wa JCB Feat Fid Q & Chid Benz, Usije Mjini wa AY & Mwana FA na Higher wa Nick wa Pili Feat Joh Makini. Wimbo Bora wa Raggae Sauti ya Rasta wa Ras Rwanda Magere, Misingi ya Rasta ya Worriers From The East, Sayuni ya Jhiko Man, Ujio Mpya ya Hardmad feat Enika & BNV, Reggae Swadakta ya Bob Lau Mwalugaja na What u Feel Inside ya Hardmad. Wimbo Bora wa Ragga/Dancehall Nimefulia wa Benjamin Mambo Jambo feat AT, Action wa CPWAA,Dully,Ngwear na Ms Trnity, Far Away ya Big Jah Man feat Richard, My Friend wa Benjamin na Kiuno weak busy ya Jet Man. Repa Bora wa Mwaka Ferguson, Khalid Chokora, Toto ze Bingwa na Kitokololo. Msanii Bora wa Hip Hop Fid Q, Joh Makini, Ngwear, Chid Benz na Godzilla. Wimbo Bora wa Afrika Mashariki Nitafanya wa Kidumu & Jay Dee, Kare wa P-Unit, Songambele wa Alpha feat AY, Vuvuzela wa Goodlife na Kasepiki wa Bebe Cool. Mtunzi Bora wa Nyimbo 20%, Barnaba, Lady Jaydee, Mrisho Mpoto na Mzee Yusuf. Mtayarishaji (producer) Bora wa Nyimbo wa Mwaka Marco Chali, Lamar, Man Water, Bob Junior na Pancho Latino. Video Bora ya Muziki ya Mwaka Mama Ntilie ya Gelly wa Ryames feat AT & Ray C, Action wa CPWAA, Dully, Ngwear, Ms Trinity, Mbagala wa Diamond na Shoga wa Shaa. Wimbo Bora wa Afro Pop Mama Ntilie wa Gelly wa Ryames feat AT & Ray C, Oyoyo wa Bob Junior, Ya Nini Malumbano wa 20%, Tamaa Mbaya wa 20% na Mbagala wa Diamond. Msanii Mpya anayechipukia Sam wa Ukweli, Linah, Sajna, Bob Junior na Top C. Wimbo Bora wa Kusirikisha/ Kushirikishwa Mama Ntilie wa Gelly wa Raymes feat AT & Ray C, Mkono mmoja wa Chege na Temba feat Wahu, Ahmada wa Offisidetrick feat Bi Kidude,Ukisikia Paah wa JC feat Fid Q & Chid Benz & Jay Moe na Dakika Moja wa FA & AY Feat Hardmad. Wimbo Bora wa Asili Tanzania Adela wa Mrisho Mpoto, Kariakoo wa Maluma, Ahmada wa Offisidetrick feat Bi Kidude,Shangazi wa Mpoki feat Cassim na Wa mbele mbele wa Ommy G. Wimbo Bora wa Zouk/ Rhumba Sina Raha wa Sam wa Ukweli, Ulofa wa Top C, Nabembelezwa wa Barnaba, Bado Robo Saa wa Amini na Bora Nikimbie wa Linah.

0 comments: