Social Icons

Monday, November 7, 2011

BoldHUYU NDIYE MISS WORLD 2011 ...

Miss Venezuela 2010 WinnersHATIMAYE kitendawili cha nani ataibuka Malkia wa Dunia 2011, kimeteguliwa kwa Miss Venezuela2011, Ivian Sarcos usiku wa Jumapili Novemba 6, 2011 kufanikiwa kutawazwa kuwa Malkia Mpya wa Taji la Urembo la dunia “Miss World 2011, hulku matumaini ya Tanzania kupitia kwa Miss Tanzania 2011, Salha Izrael Kifai yakigonga mwamba kwa mara nyingine tena katika mashindano hayo.
Vanessa Andrea Goncalves Gómez was born on February 10, 1986, in Nuestra Señora del Rosario de Baruta.
Katika shindano hilo la aina yake lililofanyika katika ukumbi wa Earls Court in London, Sarcos mwenye umri wa miaka 21 alifanikiwa kuwatupa nje zaidi ya warembo 100 kutoka nchi mbalimbali Duniani katika shindano hilo ambalo lilikuwa ni la 61 tangu kuanzishwa kwake.
Nafasi ya pili ilikwenda kwa Miss Philippines 2011, Gwendoline Ruais na nafasi ya tatu ikienda kwa Miss Puerto Rico 2011, Amanda Perez.

Bara la Afrika lilifanikiwa kuingiza warembo wawili katika hatua ya makundi ya 15 bora ambapo mrembo kutoka nchini Zimbabwe na jirani zao Afrika Kusini ndio waliolitoa kimasomaso bara hilo.
Afrika tena ikabahatika kuingia katika hatua ya 7 bora ya Miss World pale mrembo kutoka Afrika Kusini alipofanikiwa kuingia katika hatua hiyo.
Shindano hilo lilianza kufanyika saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki lilipambwa na burudani mbalimbali za muziki kutoka kundi la Vijana wa Uingereza la street dance troupe Diversity, wakifuatiwa na utambulisho wa Washiriki wote wa Miss World 2011.

Shindano hilo lilifikia tamati pale Miss World 2010 Alexandria Mills alipopanda jukwaani na kumvika taji Sarcos.
Miongoni mwa majaji wa shindano hilo alikuwa ni washindi wa taji la Miss World ambapo alikuwepo Miss World 1976, Cindy Breakspeare , Miss World 2001, Agbani Darego kutoka Nigeria,Miss World 2007, Zhang Zilin na Miss World 2009, Kaiane Aldorino.

Aidha warembo waliofanikiwa kuingia hatua ya 15 bora ni kutoka nchi za Indonesia, Korea, Italy, Sweden, Zimbabwe, Kazakhstan, Ukraine, Venezuela, Philippines, US VI, Spain, Puerto Rico, Afrika Kusini, Scotland na wenyeji Uingereza.
Huku hatua ya kundi la warembo 7 bora nafasi hizo kuchukuliwa na nchi za Korea, Venezuela, Uingereza , Philippines, Puerto Rico, Afrika Kusini na Scotland.

Saturday, November 5, 2011

KESHO HAPATOSHI LEADERS CLUB, KATIKA UZINDUZI WA ALBAMU YA DUNIA DARAJA YA TWANGA PEPETA
Hivi ndivyo vichwa vilivyoshiriki kutunga nyimbo katika albamu ya Dunia Daraja inayotarajiwa kuzinduliwa kesho ndani ya viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar es Salaam, kutoka kushoto ni Mwijuma Muumini, Saleh Kupaza, Luiza Mbutu, Dogo Rama na Chalz Baba ambaye kwa mara nyingine amebahatika kutunga wimbo unaobeba jina la albamu hiyo.
Kutoka kushoto ni Mwijuma Muumini, Chalz Baba, Luiza Mbutu, Saleh Kupaza na Dogo Rama.


KLINIKI YA SOKA YA AIRTEL RISING STARS YAFUNGWA RASMI DARMkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Shirikisho la Soka Nchini (TFF) Mtemi Ramadhani akimkabidhi Chimwemwe Birry medani katika halfa ya kufunga mafunzo ya kimataifa ya michezo katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Rashidatu Kamara akionyesha cheti alichokadhibiwa baada ya mafunzo ya soka ya kimataifa iliyofungwa rasmi jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Shirikisho la Soka Nchini (TFF) Mtemi Ramadhani akimkabidhi Chimwemwe Birry medani katika halfa ya kufunga mafunzo ya kimataifa ya michezo katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Kocha wa shule ya soka wa klabu ya Manchester United Billy Miller akimkabidhi Selemani Bofu cheti wakati wa halfa ya kufunga mashindano hayo iliyofanyika jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Selemani Bofu akipongezwa na makocha kutoka klabu ya Manchester United baada ya kuwa mfungaji bora wakati wa mazoezi ya kufunga, katikati ni Paul Bright na kushoto Billy Miller.

Thursday, November 3, 2011

'HAPPY BIRTHDAY MARIAM AZIZI'Mariam Zizi(kulia), akimrishe keki kwa kinywa chake mdogo wake ambaye ni pia miss Kurasini namba mbili 2011, Naifat Ally katika shere yake ya kuzaliwa.

JUZIKA mdau wa Mateja20, Mariam Azizi alisherehekea siku ya kuzaliwa kwake ndani ya Pub ya Cabocabana iliyopo Kinondoni B jijini Dar es Salaam, ambapo ilihudhuliwa na ndugu na jamaa zake wa karibu, sherehe hiyo ilifana vilivyo kwani watu walikula na kupombeka kwa kwenda mbele.
Mariam akimrisha keki Sada Misene.
... akimrisha shostito wake.
Keki yenye umbo la mdomo wa mtu ikiwa mezani tayari kwa mlo wa Birthday hiyo.
Miss Temeke namba tatu 2003, Mariam Omary (kushoto), akirishwa keki kwenye Birthday hiyo.
Uncle Deo naye anibugizwa kipande cha keki hiyo.
... Hassani Moshi naye ali... keki hiyo.
Mwanamuziki wa Top Band Omar Dimpoz akilambishwa kipande cha keki hiyo.
.... kweli tamuuuuuuuuuu
Mateja naye alisikilizia radha kamili ya keki hiyo.
Eeeeh! ....
Gadner ... roho ya Mariam .... akisikilizia.
Mariam & Mariam katika pozi.
...... nasiye tuilikuwepo!!!!
Kitu cha keki bhanaaaaaaa!
Omar akipozi na mtoto Mariam Bara....
Gadner katika pozi
Uncle Deo akiserebuka na miss Kurasini.
... kitu cha keki bhanaaa
Kama kawaida sehem kama hizi watu kama hawa huwa hawakosi!!!
Mambo ya misosi
Sada & Mariam
Eeeh ... tulijiachia!!
Pozi ni kama kawa sehem hizi!
Aaah!!!!! Uncle....!
Mambo ya ...
Gadner & Mariam Azizi
Wadau wakikamua katika sherehe hiyo.
Gadner & Mariam







Wednesday, November 2, 2011

MSWAADA WA KATIBA WAZIDI KUBORESHWA

Waziri Mkuu mstaafu Jaji Joseph Sinde Warioba (kulia) akitoa ushauri wa kitaalamu na uzoefu kwenye Kamati ya Sheria, Katiba na Utawala wakati wa mjadala wa Muswada wa Sheria ya Katiba ya Mwaka 2011

Baadhi ya wataalam kutoka vyombo vya Ulinzi wakiwa katika kikao hicho.


Wajumbe na wataalam mbalimbali wa Kamati ya Sheria, Katiba na Utawala, Kamati ya Mashirika ya Umma, Kamati ya Fedha za Serikali za Mitaa na Kamati ya Hesabu za Srikali wakiwa katika mijadala mikali.



Kamanda Henry Kilewo, Katibu wa mkoa wa Kinondoni Kanda ya Dar es salaam, aliyesoma tamko kali la CHADEMA jana.

MKOA WA KINONDONI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM

Tamko la katibu wa mkoa wa Kinondoni Kanda Maalum ya Dar es salaam

Ndugu zangu wanahabari,

Nimewaita hapa leo kwa lengo la kuwapa watanzania msimamamo wangu na wa chama ngazi ya mkoa kuhusu tukio la kukamatwa na kupelekwa magereza kwa Mhe. Godbless Lema Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini.
Imekuwa ikizoeleka kwa muda mrefu sasa kwamba waheshimiwa wabunge wa CHADEMA na wale wanaaotokana na vyama vya upinzani wamekuwa wakinyanyaswa sana kwa lengo la kuwafanya wajute kuingia katika siasa za upinzani Tanzania.

Hii kwa…

MKOA WA KINONDONI KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM

Tamko la katibu wa mkoa wa Kinondoni Kanda Maalum ya Dar es salaam

Ndugu zangu wanahabari,

Nimewaita hapa leo kwa lengo la kuwapa watanzania msimamamo wangu na wa chama ngazi ya mkoa kuhusu tukio la kukamatwa na kupelekwa magereza kwa Mhe. Godbless Lema Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini.
Imekuwa ikizoeleka kwa muda mrefu sasa kwamba waheshimiwa wabunge wa CHADEMA na wale wanaaotokana na vyama vya upinzani wamekuwa wakinyanyaswa sana kwa lengo la kuwafanya wajute kuingia katika siasa za upinzani Tanzania.

Hii kwa CHADEMA haitokei tu kwa waheshimiwa wabunge bali hata kwa viongozi wa ngazi zote. Inaonekana kuwa sasa serikali ya Chama Cha Mapinduzi imeamua kutekeleza kwa vitendo mkakati wa kuwatesa kwa siri na kwa wazi wale wote wanaoipinga siasa kandamizi na zisizowalazimisha watawala kuwajibika kwa wananchi.

Mkakati huu umetungwa na CCM, unasimamiwa na usalama wa taifa na unatekelezwa na jeshi la polisi. Kwa hakika hatuhoji tena kwamba jeshi la polisi ni kitengo cha kusimamia maamuzi na maelekezo ya CCM badala ya kulinda raia na mali zao.

Mheshimiwa Godbless kama mbunge wa wananchi wa jimbo la Arusha Mjini amekuwa akifuatwafuatwa na jeshi la polisi kila mara na kufanyiwa vitendo vingi vya udhalilishaji na unyanyasaji hasa kwa kupitia OCD wa Arusha Mjini Zuberi.

Mathalani wiki iliyopita siku ya ijumaa tarehe 28/10/2011 Mhe. Godbless lema akitoka mahakamani alisindikizwa na wananchi wake kutoka mahakamani hadi ofisini kwake. Wafuasi wake walipomfikisha ofisini waliondoka na kurejea makwao. Huko ofisini aliwakuta wananchi wakimsubiri ili awahudumie kama mbunge wajimbo lao. Wakati akiongea na wananchi ghafla polisi walifika na kuwakamata wananchi wote waliokuja kuomba usikivu wa mbunge na kuwapeleka kituo kikuu cha polisi.

Mbunge Lema alipokwenda kituo cha polisi kwa lengo la kuwawekea dhamana naye aliwekwa chini ya ulinzi kwamba eti amefanya maandamano bila kibali.

Tunahoji: Ni maandamano yapi hayo ambayo Lema aliyafanya na wananchi wake akiwa angali ofisini kwake? Je maandamano wanayoyazungumzia ni kuondoka na wananchi mahakamani hadi ofisini kwake? Je kama kuondoka kwake na wafuasi wake mahakamani ni kosa kisheria; Je kwa Mhe Ole Sendeka alipokuwa akitoka mahakamani, alikuwa akiondoka na kundi kubwa la wafuasi wake na kusindikizwa na OCD huyu huyu? Vile vile Mwenyekiti wa UV-CCM mkoa wa Arusha amekuwa akienda kituo kikuu cha polisi akisidikizwa na kundi kubwa la wafuasi wake wa CCM. Polisi hawakuwahi kuwakamata wala kuwaonya. Sasa haya yote yalikuwa maandamano ama matembezi ya hisani? Maana Arusha kuna msiba mkubwa wa CCM kukataliwa na wananchi.

Kwa hakika tukio la kukamatwa kwa Mhe Lema, kupelekwa mahakamani na hatima ye kupelekwa gerezani ni ushahidi wa kutosha kwamba jeshi la polisi sasa linakamilisha sehemu kubwa wa wajibu wake wa kuibaka demokrasia.


Hata hivyo tunalitaka jeshi la polisi na serikali ya CCM wajue kwamba kitendo cha kumpeleka Lema magereza ni ushindi tosha katika harakati za ukombozi wa taifa hili. Maana hakuna silaha yoyote duniani ama jeshi la polisi popote pale duniani ambavyo viliweza kushinda vita dhidi ya ukweli, haki na uwazi.

Ndugu zangu watanzania

Tunawaunga mkono wana Arusha kwa kumpata mbunge ambaye anayatetea maslahi yao kwa mzigo hata pale inapobidi kwenda gerezani kwa ajili ya watu wake na hata ikibidi kifo anaweza kusimamia hilo. Alisema Martin Luther King Jr. 1963 “A man who wont die for something is not fit to live” na akaendelea kusisitiza “Nobody can give you freedom, nobody can give you justice or right or anything.

You take it!” (STAND UP; STAND UP 4, UR RIGHT) Hayo yalikuwa maono ya bob marley ambayo aliyaona mwaka wa 1973,baada ya kuwa amekaa katika mto mmoja huko jamaica akaona samaki wanapita katika maji lakini samaki wakubwa wakawa wanawaonea samaki wadogo,hivyo akaona hata hapa duniani hata wa2 walio juu wanawaonea watu wa hali ya chini.

Kwa watu wanaopinga ama kukejeli maamuzi ya Godbless lema kukataa dhamana, Wathubutu kufanya ziara huko Mahospitalini wavae sura za uhasilia wa kibinadamu wakaone watu waliokuwa kama wao jinsi wanavyotaabika kwa kukosa matibabu ile hali ni walipa kodi wa taifa hili. Kwanini Godbless asiende jela wakati anasimamia mambo ya msingi na hayatekelezwi, tukiandamana tunaonekana tunavunja sheria ni afadhali kwenda sehemu wanayodhani tunaogopa kuliko kukaa kimya kumbe hatuogopi. Mungu yupo upande wetu na tunaelekea kushinda unyanyaswaji huu.

Kama ambavyo alivyowahi kusema Martin Luther king jr, ndivyo tunavyo wahakikishia wana wa Arusha, we will work together; we will stand up together, we will go to jail together, until justice runs down like water. maana mateso tunayoyapata ni makubwa kuliko huko jehanam tusipopajua.

Kwa kuonyesha tuko pamoja katika harakati hizi za kudai demokrasia ya kweli tunampogeza Godbless lema mbunge wa Arusha mjini kwa kupeleka ujumbe kwa watawala wanaodhani wanaweza kutumia magereza kama sehemu ya vitisho kurudisha harakati zozote zile nyuma.


Ujumbe huu uwafikie watawala yakuwa jela sisehemu ya kumtishia mtu yeyote Yule mwenye akili timamu, mpenda haki bali ni sehemu ya kawaida ambapo binadamu yeyote Yule anaweza kwenda.

ASANTENI ASANTENI NA MUNGU AWABARIKI WATANZANIA WENZANGU!

Henry J Kilewo
KATIBU (M) Kanda Maalum
01/11/2011