Tuesday, August 10, 2010
BASATA
Monday, August 9, 2010
RAHA ZA FIESTA 2010
Mbali na ukubwa, ‘matirio’ ya jukwaa hilo kuanzia uimara wake, taa na vinginevyo, ni sifa ambazo zinalitofautisha na mengine yaliyotumika nchini.
Hata hivyo, chanzo cha warembo hao kutwangana wakati shoo ya Fiesta 2010 ilipokuwa imepamba moto hakijajulikana, lakini ‘mtiti’ wao ulikuwa si wa kitoto.
Lil Kim aliyeanza kutisha tangu miaka ya 90 akiwa na ‘lebo’ ya Bad Boy Entertainment na kuvuma kwa uhusiano wake wa kimapenzi na mwana Hip Hop, marehemu Christopher Wallace ‘Notorious BIG’, alionesha kuelewa hadhira ya Bongo inataka nini na akaipa.
Kupanda kwa Nature jukwaani na kupiga shoo ya pamoja na Lil Kim, ilikuwa ni mseto wa ambao haujawahi kutokea, hivyo kusababisha shangwe za kiwango cha juu.
Uhodari wa Lil Kim katika kucheza staili ya ‘Mapanga Shaa’, wepesi wa kunengua wimbo wa Nature wa ‘Mugambo’ na kadhalika, ni vitu ambavyo vilimuongezea mwanamuziki huyo alama za kushingiliwa.
Kim, alizidi ‘kuiroga’ hadhira pale alipokuwa anamkumbatia Nature mara kwa mara na kumpiga mabusu, ‘manjonjo’ ambayo yaliamsha kelele.
Kionjo kingine ni kivazi cha Kim ambacho muda wote kilianika kufuli lake, hivyo kuwafanya baadhi ya wenye uchu, kupiga chabo chini ya jukwaa.
Kituko kingine ni mdau wa soka, Nagari Kombo aliyefanya kituko Mei mwaka huu kwa kuingia Uwanja wa Taifa na kumkumbatia staa wa Real Madrid, Mbrazil Ricardo Kaka wakati Timu ya Soka ya Taifa la Tanzania ‘Taifa Stars’ ilipocheza na Brazil, kushtukiwa kwenye jaribio la kumvaa Kim.
Stadi wa Hip Hop Bongo, John Simon ‘Johmakini’ alidhihirisha umwamba wake wa Kaskazini na kuonesha kuwa ‘swaga’ anazijua kwa kupiga shoo ya kiwango bora.
Wasanii wengine wa Bongo waliotisha jukwaani ni Fareed Kubanda ‘Fid Q’, Wanaume Family, Witness Kaijage, Hamis Mwinjuma ‘MwanaFA’, Sara Kaisi ‘Shaa’, Nassib Abdul ‘Diamond’, Kikosi cha Mizinga, Barnaba na Linah (THT).
Staa wa Misifaz Camp, Abdul Sykes ‘Dully’ hakufanya vizuri jukwaani kutokana na kile ambacho kilibeba tafsiri kwamba amekuwa bonge na uzito kuongezeka.
Wakali kutoka Ivory Coast, DJ Rahmatullah na mwimbaji wa staili ya Aladji, walitegemewa wangefunika lakini ilikuwa kinyume, kwani walifunikwa na wanamuziki hata wa nyumbani.
Kundi la Brackets la Nigeria, nalo lilifanya vizuri kwa kugonga ‘mchanyato’ wa nyimbo zao za zile za Kundi la P-Square.
Kwa jumla, shoo nzima ilipangiliwa vizuri kuanzia mwanzo majira ya saa 9 alasiri (Jumamosi) hadi saa 11 alfajiri (Jumapili).
Timu ya Ijumaa Wikienda iliyofanya ‘kavareji’ Fiesta ni Sifael Paul, Richard Bukos, Musa Mateja, Aziz Hashim, Hemed Kisanda na Shakoor Jongo.
Friday, August 6, 2010
WADHAMINI FIESTA WATOA VYANDARUA, RANGI HOSPITALI YA M/NYAMALA POLISI OYSTER BAY
TIMU inayosimamia mpango wa burudani wa Fiesta kutoka Clouds FM chini ya udhamini wa Kampuni ya Bia ya Serengeti leo imetoa msaada wa vyandarua dhidi ya malaria vipatavyo 300 na rangi za kupaka majengo zenye thamani ya shilingi milioni 5.5 kwa Hospitali ya Mwananyamala na kituo cha Polisi cha Oyster Bay jijini.
Baadhi ya wasanii na waandishi wa habari wakielekea katika vyumba vya wagonjwa tayari kwa kuwapa pole.
Kassim Mganga akiwa ameshikilia kifaa cha usafi tayari kwa kazi hiyo.
Mwanamuziki wa Bongo, Angelis Faber (Enji) akifanya usafi mahali hapo.
Msanii wa Filamu nchini Elizabeth Michael ‘Lulu’ akiwa kwenye pozi.
Wednesday, August 4, 2010
BINGWA WA KUTEMBEA JUU YA KAMBA!
Kutana na kijana bingwa wa kutembea juu ya kamba na kisha kuvua na kuvaa suruali juu kwa juu bila kudondoka!
Raaaaaaa!!! Ilivyochengua CCM Kirumba Mwanza
Jana Jumapili ilikuwa ni siku ya wakazi wa Mwanza kujipangusa Raaaaaah na Fiesta 2010 kwa kushuhudia shoo kali kutoka kwa wasanii wakali wa muziki wa Bongo Flava na Hip Hop. Pichani ni kinara wa Hip Hop from Rock City, Fid Q akipelekesha mashabiki wake.
Diamond akiwaimbisha wakazi wa Mwanza wimbo wake wa Mbagala ambao umefanya vyema kwa kiasi kikubwa.
Anaitwa Bell 9,kichwa kingine katika anga ya muziki wa bongofleva kikitokea mkoani Moro,akiwarusha washabiki na wapenzi wake waliofurika ndani ya uwanja wa ccm kirumba kupitia wimbo wake wa Masogange na nyinginezo jioni ya jana.
Brazameni Dully Sykes a.k.a Mr Misifa kaiwarusha mashabiki wake.
Rrrhhaaaa zikizidi mpango mzima huwa kama hivi,chini juu,juu chiini aahh freeshh.!
Sugu Mbeya, kama Dk. Slaa Karatu
Vijana hao, waliizingira ofisi ya CHADEMA mkoa, wakimtaka Sugu atoke nje ili watembee naye kwa miguu kwa maelezo kwamba maelefu ya wakazi wa mkoa huu, walikuwa mitaani wakimng’oja.
Hakuna kupanda gari kaka, tunatembea wote kwa miguu. Tunataka kupeleka misukosuko mitaani. Wewe ndiye mbunge wetu,” alisikika kijana mmoja, aliyekuwa jirani zaidi na mlango wa ofisi ya chama.
Hata hivyo, jaribio hilo la vijana kutembea na Sugu mitaani, lilizimwa na Katibu wa CHADEMA mkoa, Edo Makata ambaye aliwaambia kwamba hairuhusiwi kufanya hivyo kwa sababu itaonekana chama kimeanza kampeni mapema.
Mwenyekiti wa CHADEMA, Mbeya Mjini, John David Mwambigija, naye alikuwa kwenye wakati mgumu, alipokuwa akiwatuliza vijana hao kuelewa sheria za uchaguzi, kwani wengi wao hawakutaka kumuelewa kabisa.
Sugu, alipozungumza na gazeti hili, alisema kuwa hamasa ya wakazi wa Mbeya, inampa changamoto ya kuwatumikia kwa nguvu na kwamba hatoruhusu uozo wowote.
“Nafarijika sana kwa jinsi ninavyoungwa mkono. Ndani ya muda mfupi, nimekubalika mno kisiasa. Nitafanya nao kazi na kuwatumikia kwa nguvu zote baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa Mbeya Mjini. Kila kitu kuhusu kujitangaza, nasubiri muda wa kampeni,” alisema Sugu.

