Social Icons

Monday, July 19, 2010

TUZO ZA ZIFF; MONALISA, KAMAU WANG’ARA

Monalisa akikabidhiwa tuzo na Martin Mhando, Mkurugenzi wa ZIFF.
USIKU wa kuamkia Jumapili iliyopita, event ya utoaji tuzo katika Tamasha la Kimataifa la Filamu la ZIFF, ilichukua nafasi katika ukumbi wa Ngome Kongwe, mjini Zanzibar ambapo filamu na wasanii waliofanya vizuri walitunukiwa tuzo.

Miongoni mwa wasanii na filamu zilizong’ara, ni filamu ya Ndoto za Elibidi kutoka Nchini Kenya, iliyotungwa na Kamau wa Ndung'u na Nick_Reding ambayo ilinyakua jumla ya tuzo nne, wakati msanii Yvone Cherry Monalisa alikuwa msanii pekee wa kibongo aliyenyakua tuzo ya mwigizaji Bora.

Tuzo nyingine zilizotolewa ni pamoja na Themba (Best Feature Film-Golden Dhow), Imani (Best Feature Film –Silver Dhow), The Gift (Filamu fupi bora), Pumzi (Special Jury Prize), Motherland( Best Documentary), Ndoto za Elibidi (Verona Award), Soul Boy (SIGNIS award), A step into darkness (SIGNIS Award) na My City on fire (East African Talent Award) kutoka Uganda.

Wengine ni Shungu (Sembene Ousmane Award), The gardener and his 21 flowers (Sembene Ousmane Award), My Policy (Chairman Award), Nani (Best Tanzanian Film), wakati tuzo ya Lifetime Achievement ikienda kwa Profesa Elias Eliezer Jengo na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Zanzibar, Mahmoud Thabit Kombo ambaye aliondoka na tuzo ya ZIFF Ambassador.


Kamau wa Ndung’u na Nick Reding wakifurahia tuzo waliyoipata kutokana na filamu yao ya Ndoto za Elibidi.


Mzee Chilo naye alikuwepo eneo la tukio, hapa akiwa amechill na Monalisa.


Mtunzi wa filamu ya Shungu akipokea tuzo yake.


Wanuri Kahiu kutoka Kenya tuzo baada ya filamu yake ya pumzi kuibuka kidedea.


Wasanii wa filamu wa kibongo waliohudhuria kwenye tamasha la ZIFF wakiwa jukwaani.


Mtunzi wa filamu ya Nani, Sajni Srivastava akiifurahia tuzo yake.


Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wa Zanzibar, Mahmoud Thabit Kombo ndiye aliyekuwa mgeni rasmi.


Mtunzi wa filamu ya My City on Fire, Dennis Onen akiifurahia tuzo aliyoipata.


PICHA NA HASHIM AZIZ / GPL ZANZIBAR

SHUMILETA ASHEREKEA KI STAILI BIRTH DAY YAKE!

jana ilikuwa ni siku ya kuzaliwa staa wa kike wa filamu za Bongo maarufu kwa jina la SHUMILETA...aliandaa kijisherehe chake pale Lamada Hotels & Apartments Ilala ambako alikusanya mashoga zake na kujilia mkeki aliokuwa amewaandalia....huku akijivunia kufikisha 27 yrs duniani..!

mkeki huo....


akimlisha shoga yake Jaque

...akimlisha shoga yake Rungi

....na yeye akijisevia....ammmh!!!

....mmmmh tamuu!!!

...akiwa na washikaji zake

..pozi la Jaque baada ya kula mkeki

waswahili husema penye mtama njiwa hawakosekani.....Victor wa Buguruni huyo!!!!


Thursday, July 15, 2010

MAUJI KWENYE BAA MCHANA KWEUPE!

Kijana mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Sadam ameauwa kwa kupigwa risasi mchana wa leo katika baa maarufu ya Angels' Park iliyoko Ilala Sharief Shamba jijini Dar es salaam!! Kijana huyo inadaiwa kuuawa na mmiliki wa bar hiyo baada ya kundi la vijana wengi, akiwemo marehemu, kuvamia kwa lengo la kumpiga mwenye baa ili kulipiza kisasi! Mtandao huu umeeleza na mashuhuda kuwa, sakata lilianzia jana baada ya vijana wasiojulikana kudaiwa kumkaba mteja mmoja wa baa hiyo akiwa chooni na vijana hao kukamatwa na kuplekwa polisi ambako walishikiliwa hadi leo. Imedaiwa kuwa baada ya kuona wenzao wanasota rumande, pengine kwa sababu ya mmiliki wa huyo, waliamua kumfuata ili kulipiza kisasi kwa kumfanyia.

Wakiwa kundi huku wameshika silaha mbalimbali vikiwemo visu, vijana hao walivamia baa hiyo na kuanza kumpiga mwenye baa na kumchoma kisu ambacho bahati nzuri hakikumdhuru sana. Kuona hali hiyo, mwenye baa alitoa bastola yake, akapiga hewani ili kuwatisha, lakini waliendelea kumfuata na kumshambulia huku wakiharibu mali za baa hiyo, likiwemo gari lake lililovunjwa kioo cha nyuma. Awali vijana wawili walipigwa risasi na kujeruhiwa na marehemu aliendelea kumfuata mwenye baa na ndipo alipopigwa risasi na kufa papo hapo!

...sehemu ya watu waliojazana kushuhudia tukio hilo la aina yake kuwahi kutokea mitaa ya Ilala!

...jamaa wakibeba maiti ya Sadam kuingiza kwenye gari la polisi

...

...gari la mwenye baa lililovunjwa vioo na vijana hao wakati wakivamia baa hiyo


JK ZIARANI JIMBONI KWA SPIKA

Mh. Rais J.K akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuzindua rasmi Ofisi ya Mbunge wa Urambo Mashariki, Mh. Samuel Sitta, (aliyesimamam ) ambaye pia ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


WANANCHI WENYE HASIRA

Kwa mara nyingine tena, kile kinachoelezwa kama 'wananchi wenye hasira, kimefanya kazi yake tena baada ya kumchoma moto wa tairi kijana aliyedhaniwa kuwa kibaka. Jamaa anaonekana kijana mmoja akimsaidia Israel kutoa roho ya kibaka huyo aliyedaiwa kutaka kuiba baiskeli kwenye nyumba ya mkazi mmoja maeneo ya Mabibo jijini Dar es Salaam leo alfajiri. Jina la kijana huyo halikuweza kufahamika mara moja.


Kijana aliyedaiwa kuwa kibaka akiteketea kwa moto na kipigo huku akiwa amevishwa tairi.


….Kibaka akiteketea! .Dah!


PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL

VITUKO VYA CHARLES BABA!

Charles Baba, mwimbaji mahiri wa Twanga Pepeta anasema anahusudu sana Tatoo na ndiyo maana mwilini mwake zimejaa kibao. moja ya tatoo hizo ni hii hapa...mwenyewe anadai ni sura ya YESU...is it?

taoo la mkono mzima

siyo kama anauza viatu vya mitumba, la hasha, hivi ni sehemu ya lundo la viatu alivyonavyo ambalo alikutwa nalo kwenye gari lake akidai anapeleka kwa SHOE SHINER...anadai kila wiki hununua kiatu kipya na kuacha cha zamani...sasa amevikumbuka!!


Tuesday, July 13, 2010

MATONYA KURUDI DAR KWA KISHINDO! -globalpublishers reports

Matonya akiwa mtaani.

Na Dunsata Shekidele,Morogoro.
OMBA omba maarufu nchini, Anthony Matonya, ambaye kwa sasa ameweka maskani katika mitaa ya Morogoro mjini, amesema kwamba yuko kwenye mchakato wa kurudi jijini Dar es salaam baada ya kuona wakazi wa mkoa huo wamemzowea sana kiasi cha kumkejeli badala ya kumsaidia.

Matonya aliyasema hayo leo asubuhi ofisini kwake barabara ya madaraka eneo la Msikiti wa Jamatini alipofanya mahojiano maalumu na mwandishi wetu juu ya mustakabali wa maisha aliyokuwa akiishi jijini Dar es salaam na yale anayoishi mkoani hapa.

"Swali zuli sana umeniuliza, ukweli maisha ya hapa Morogoro kwa sasa nayaona ni magumu, hilo linatokana na watu wengi wa hapa kiunizoea na kunipita bila kunipa chochote huku wakisema kwamba hawanisaidi kwa kuwa mimi ni maarufu nchini kuliko wao, hivyo hali hiyo ya umaarufu wa kijinga inanigharimu katika kipato changu. kwa sababu hiyo, niko kwenye mchakato wa kurejea jiji Dar es salaam, nadhani kwa sasa kumepoa kidogo tofauti na wakati ule wa serikali ya Makamba,"alisema Matonya.


Matonya akikinga kopo lake kupokea kitu kidogo kutoka kwa mpita njia

matonya akiwa kazini, huku wapita njia wakimshangaa

MWALIMU APATA AIBU YA MWAKA MBELE YA WANAFUNZI WAKE!

Mwalimu Agnes (aliyekaa) akishushuliwa na mume wa Jamila akiwa shuleni tena mbele ya wanafunzi wake wa shule ya Msingi Mchangani iliyopo Mwananyamala, jijini Dar es salaam baada ya kudaiwa kumuibia mkoba shoga yake aliyemfuata nyumbani kwake kumuuzia...ilikuwa ni aibu ambayo walimu wenzake waliamua kumchangia sh 32,000 thamani ya mkoba huo ili kuepusha soo zaidi...mkasa kamili fuatilia kwenye gazeti la Ijumaa ya wiki hii hapa hapa mtandaoni..!

Shigongo aongea na Watanzania Marekani

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers, Eric Shigongo ameongea na Watanzania waishio nchini Marekani na kuwataka kuchangia maendeleo ya Tanzania na kuwa na mtizamo mwingine kuhusu nchi yao.

Akihutubia katika mkutano wa Diaspora 2010 uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Marriot Hotel, Minneapolis nchini Marekani wiki iliyopita, Shigongo alisema mafanikio hayawezi kupatikana nchini Marekani peke yake kama ambavyo vijana wengi wanadhani, bali palipo na nia kila kitu kinawezekana mahali popote bila kujali historia ya mtu wala kiwango cha elimu alichonacho.

Aliwataka vijana walioko nje kubadilisha mtazamo wao kuhusu Tanzania kwani wengi wao wamekuwa na fikra hasi kuhusu nchi yetu na wamekata tamaa.

“Ni kweli inawezekana baadhi ya mambo yanayofanywa na watu wachache nchini yanavunja mioyo na kukatisha tamaa, lakini, je, ndiyo tuache mambo yaendelee yalivyo au tuyaweke yanapotakiwa kuwa? Ni kosa kubwa sana kuikatia tamaa nchi yetu wenyewe.

“Mungu alituweka pale (Tanzania) kwa makusudi, hivyo ni lazima kila mmoja wetu, mkubwa kwa mdogo kuhakikisha tunachangia maendeleo ya nchi yetu hata kama ni kwa kutonyamazia maovu yanayofanywa na wachache, lazima tuwe tayari kujitoa mhanga kwa ajili ya vizazi vijavyo kama walivyofanya walioishi kabla yetu ambao hata majina yao hayatajwi katika historia,” alisema Shigongo.

Aidha, aliwataka vijana kufumbua macho na kuziona nafasi tele za kufanikiwa zilizopo nchini mwetu badala ya kupishana na Wachina pamoja na Wazungu uwanja wa ndege wakija kuchukua kila kitu ambacho kingewafaa Watanzania.

“Huu ndiyo wakati wa nyinyi kuja nyumbani kuchangamkia nafasi za mafanikio kabla hazijaisha, huko tunakokwenda, kama mambo hayatabadilika, itakuwa vigumu sana kwa Watanzania kufanikiwa, nafasi inazidi kuwa finyu kadri tunavyozidi kupanda juu,” alisema Shigongo huku akimtaka kila mmoja kuwa na mchango kwa maendeleo ya nchi yetu.

Alisema kufanya hivyo na huku serikali ikitimiza wajibu wake, Tanzania haitabaki ile ile miaka michache ijayo, na kwamba tufanye kazi kwa uzalendo huku tukiwafikiria watakaokuja baada yetu.

Katika mkutano huo ulioandaliwa na Baraza la Watanzania waishio nchini Marekani (DICOTA), wawekezaji wa makampuni makubwa nchini Marekani kama vile General Mills walikuwepo kukutana na Watanzania. Viongozi wengine kutoka Tanzania waliopata nafasi ya kuzungumza ni pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo ambaye aliwahakikishia Diaspora kuwa serikali ya Tanzania iko tayari kuwasaidia pale watakaporejea nyumbani kuchangia maendeleo yetu.

Aidha, Kamishna wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), Harry Kitilya naye aliongelea juu ya misamaha ya kodi inayotolewa kwa Watanzania walioko nje ya nchi pale wanaporejea nyumbani na alipongezwa kwa uamuzi wake wa kukifunga kitengo cha Long Room kilichodaiwa kuwa na usumbufu mkubwa na kuwa chanzo kikubwa cha rushwa na kushuka kwa mapato ya serikali.

Mwakilishi wa CRDB Bank katika mkutano huo, alifafanua kuhusu akaunti yao ya Tanzanite na Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji nchini (TIC), Emmanuel Ole Naiko aliongelea juu ya umuhimu wa kuwekeza nyumbani. Halikadhalika, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Dhamana ya Uwekezaji, Dk. Hamis Kibola alihudhuria mkutano huo.

Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Ombeni Sefue na kamati nzima ya DICOTA, ikiongozwa na Dk. Lennard Tenende, ilipongezwa na wajumbe waliohudhuria mkutano huo kwa maandalizi mazuri ambapo Kampuni ya Global Publishers ilipewa tuzo kwa kazi nzuri inayoifanya katika jamii ikiwa ni pamoja na kuwa miongoni mwa wadhamini wa mkutano huo.

ANTI EZEKIEL AFIWA!

Mcheza filamu wa Bongo, Aunti Ezekiel, amefiwa na wifi yake aitwaye Habiba, ambaye alikuwa ni mke wa kaka yake, Mande Ezekiel. Mazishi yamefanyika jioni hii katika makaburi ya Mtoni Kijichi ambako mtandao huu ulikutana na msanii huyo akiwa na baadhi ya shoga zake wakitoka makaburini.

Anti akipewa pole na shoga yake, Fideline Iranga

Saturday, July 3, 2010

ALICE ATWAA TAJI LA MISS KINONDONI


Mtanange wa kumsaka mrembo wa jimbo la Miss Kinondoni 2010/11 jana ulimalizika katika ukumbi wa Mlimani City ambapo mrembo aliyekuwa amevaa namba ya ushiriki 4 Alice Lushiku ndiye aliyetwaa taji hilo huku namba mbili ikinyakuliwa na Irene Hezeron na Amisuu Umari akikamilisha safu ya tatu bora kwa nafasi hiyo.



Warembo waliyokuwa wakiwania taji hilo wakiwa mbele ya watazamaji.



Mkufunzi wa warembo Joketi Mwegelo (kulia), akimpatia swali la kujibu Alice Lushiku ambalo alijibu vizuri na kumuongezea ‘point’ za ushindi.


Miss Kinondoni aliyemaliza muda wake, Lulu Abraham (kulia) akimvisha taji kwa mmliki mpya wa taji hilo, Alice baada ya kuwabwaga wenzake 10 na kutangazwa mshindi.



Wanenguaji wa Bendi ya African Stars International ‘Twanga Pepeta’ wakiwajibika stejini katika kinyang’anyiro hicho.

Miss Kinondoni 2010 Alice Lushiku (katikati) akiwa kwenye pozi la pamoja na warembo wenzake waliyoshika nafasi za juu (kushoto)ni Irene Hezeron aliyeshika namba mbili mwishoni kulia ni Amisuu Umari aliyeshika namba tatu.

Alice akiwa kwenye pozi baada ya kutwaa taji.

Friday, July 2, 2010

HAA! AISHA MADINDA UNAMCHEKA INTERNET!

Mnenguaji namba moja ndani ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ Aisha Madinda hivi juzi kati alinaswa na kamera yetu katika viwanja vya Leaders Club akichekelea baada ya kupiga picha ya pozi na Lilian Tungaraza ‘Lilian Internet’

FAGASON NA WANAYE JUKWAANI!


Rapa maridadi wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta International’ Saulo John ‘Fagason’ alisherekea hivi miaka kumi ya albam za Bendi hiyo.

EEH!BRO’ NAWE HAUVUMI LAKINI UMO!

Brother man huyu amba jina lake harikupatikana haraka hivi karibuni kamera yetu ilimnasa akijiachia na mrembo ndani ya Ukumbi wa Travertine Maomeni jijini Dar